New Orleans ni mji wa Marekani katika jimbo la Louisiana. Ni mji mkubwa wa Louisiana ukiwa karibu na mdomo wa mto Mississippi unapoishia katika Ghuba ya Meksiko. Mji uko kati ya mto na ziwa kubwa la Lake Pontchartrain.
Hadi Julai 2005 ilikuwa na wakazi 454,863 ikaathiriwa vibaya na tufani "Katrina" iliyoharibu sehemu kubwa na idadi ya wakazi imepungua hadi kufikia 223,388 katika mwaka 2007.