Njia ya reli ni barabara maalumu iliyojengwa kwa ajili ya matumizi ya treni.
Kwa kawaida njia hii hutengenezwa kwa kufunga pau mbili za feleji sambamba kwenye mataruma ya mbao, simiti au chuma zinazokaa juu ya msingi wa mawe ya kokoto.
Umbali kati ya reli mbili umesanifishwa katika kila nchi au angalau eneo la kampuni ya reli. Umbali huo unapaswa kulingana kikamilifu na upana wa magurudumu ya treni maana tofauti na magari barabarani treni hazilengwi na dereva bali na reli za njia zenyewe.