Papa Adrian VI

Papa Adrian VI alivyochorwa na Jan van Scorel.
Papa Adrian VI alivyochorwa mwaka 1568.
Nyumba ya kuzaliwa ya Papa Adrian na shairi linaloandamana. Maelezo ya mchongo wa 'Wanaume na Wanawake Maarufu wa Uholanzi'.

Papa Adrian VI (2 Machi 145914 Septemba 1523) alikuwa Papa kuanzia tarehe 9 Januari/31 Agosti 1522 hadi kifo chake[1]. Alitokea Utrecht, Uholanzi[2]. Alikuwa Mholanzi pekee kuwa Papa, na alikuwa Papa wa mwisho asiye Mwitalia hadi Papa Yohane Paulo II kutoka Polandi alipochaguliwa miaka 455 baadaye [3].

Jina lake la kuzaliwa lilikuwa Adriaan Florensz, hivyo hakubadili jina la ubatizo alipochaguliwa kuwa Papa, tofauti na watangulizi na waandamizi karibu wote wa milenia ya pili.

Alimfuata Papa Leo X akafuatwa na Papa Klementi VII.

  1. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  2. https://www.vatican.va/content/vatican/en/holy-father.index.html#holy-father
  3. Gerard Weel Life and times of Adrian of Utrecht Archived 25 Oktoba 2014 at the Wayback Machine (in Dutch)

Papa Adrian VI

Dodaje.pl - Ogłoszenia lokalne