Patrice Lumumba

Picha halisi ya Patrice E. Lumumba.

Patrice Lumumba (2 Julai 192517 Januari 1961) alikuwa mwanasiasa na kiongozi wa uhuru wa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Mwaka wa 1958 alikuwa miongoni mwa waanzishaji wa Chama cha Taifa la Kongo (kwa Kifaransa: Mouvement National Congolais).

Mwaka wa 1960 alipata kuwa Waziri Mkuu wa kwanza wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo baada ya kuongoza harakati za kugombea uhuru toka kwa utawala wa kikoloni wa Wabelgiji.

Baada ya miezi miwili tu ya kuwa Waziri Mkuu, Lumumba alipinduliwa na baadaye kutiwa ndani kabla ya kuuawa katika mazingira ya kutatanisha katika eneo la Katanga upande wa kusini wa Kongo.


Patrice Lumumba

Dodaje.pl - Ogłoszenia lokalne