Planktoni (Kigiriki πλαγκτος planktos "inayoelea kwenye maji") ni jina la kujumlisha viumbe vidogo sana ama mimea au wanyama wanaoishi baharini. Wadogo jinsi walivyo hawana nguvu kuogelea dhidi ya mikondo ya bahari kwa hiyo wanaelea tu baharini wakisukumwa na mwendo wa maji.
Planktoni ni chanzo cha maisha ya viumbe vingine kama samaki hadi wanadamu wanokula samaki au kulisha mifugo yao unga wa samaki.