Radi (elementi)

Kwa ngurumo ya umeme tazama radi


Radi
Jina la Elementi Radi
Alama Ra
Namba atomia 88
Uzani atomia 226,0254 u
Valensi 2, 8, 18, 32, 18, 8, 2
Ugumu (Mohs) {{{ugumu}}}
Kiwango cha kuyeyuka 973 K (700 °C)
Kiwango cha kuchemka 2010 K (1737 °C)
Saa hii yasomeka gizani kwa sababu ya nukta kwenye namba na kwenye mikono yake hung'aa gizani kutokana na radi kwenye rangi ya kijani na nukta hizi.

Radi (kutoka Kilatini "radius") ni elementi katika mfumo radidia yenye alama Ra.

Namba atomia ni 88 na uzani atomia ni 226.0254.

Jina limechaguliwa kutokana na tabia yake ya ununurifu: kwa Kilatini "radius" yamaanisha "mwale" au "mwonzi".

Kikemia radi ni metali ya udongo alikalini yenye rangi nyeupe. Lakini inaoksidisha haraka kushika rangi nyeusi.

Radi ni haba sana hutokea kama sehemu ya mchanganyiko wa madini kadhaa pamoja na urani. Hutokea hasa kama isotopi ya 226Ra yenye nusumaisha ya miaka 1,602 ikibadilika kuwa gesi ya radoni.


Radi (elementi)

Dodaje.pl - Ogłoszenia lokalne