Tetekuwanga | |
---|---|
Mwainisho na taarifa za nje | |
Kundi Maalumu | Infectious diseases, pediatrics |
ICD-10 | B01. |
ICD-9 | 052 |
DiseasesDB | 29118 |
MedlinePlus | 001592 |
eMedicine | ped/2385 derm/74, emerg/367 |
MeSH | C02.256.466.175 |
Tetekuwanga, tetewanga au tetemaji (kwa Kiingereza chickenpox, kitaalamu varicella) ni ugonjwa wa kuambukiza sana unaosababishwa na maambukizo ya kimsingi ya virusi vya varisela zosta (VZV).[1] Kwa kawaida huanza kwa vipele vya lengelenge kwenye ngozi, hasa mwilini na kichwani wala si pembeni, na hugeuka kuwa makovu mabichi, yanayowasha, ambayo aghalabu hupona bila kuacha mabaka.
Tetekuwanga huenea kwa urahisi kwa njia ya ukohozi au kwenda chafya au kuingiliana moja kwa moja na watu wanaougua walio na vipele vinavyovuja. Baada ya maambukizi ya mwanzo, kwa kawaida, kinga ya kudumu maisha hujengeka dhidi ya matukio ya baadaye ya uambukizwaji tetekuwanga.
Tetekuwanga ni nadra kuua, ingawa kwa ujumla huwa kali zaidi kwa watu wazima wa kiume kuliko wanawake ama watoto. Wanawake wajawazito na wale wenye mfumo wa kingamaradhi uliopunguka huwa katika hatari zaidi ya kutatizika pakubwa.
Tetekuwanga kwa sasa inaaminika kuwa sababu ya theluthi moja ya matukio ya kiharusi kwa watoto.[2] Tatizo la kawaida zaidi kutokana na matukio ya tetekuwanga ya baadaye ni vipele, vinavyosababishwa na muathiriko mpya wa virusi vya varisela zosta baada ya miongo tokea matukio ya awali ya tetekuwanga.
Tetekuwanga imeonekana pia katika viumbehai wengine, wakiwa pamoja na tumbili[3] na masokwe.[4]
{{cite journal}}
: Unknown parameter |month=
ignored (help)
{{cite journal}}
: |access-date=
requires |url=
(help); Unknown parameter |month=
ignored (help)CS1 maint: multiple names: authors list (link)
{{cite journal}}
: |access-date=
requires |url=
(help); Unknown parameter |month=
ignored (help)CS1 maint: multiple names: authors list (link)