Noël Isidore Thomas Sankara (* 21 Desemba 1949 mjini Yako, Volta ya Juu; † 15 Oktoba 1987 mjini Ouagadougou, Burkina Faso) alikuwa mwanajeshi na mwanasiasa nchini Burkina Faso. Kuanzia 4 Agosti 1983 hadi kuuawa kwake tarehe 15 Oktoba 1987, Sankara alikuwa rais wa tano wa Volta ya Juu aliyoibadilishia jina kuwa Burkina Faso.