Ualimu wa Kanisa katika imani ya Wakatoliki linamaanisha mamlaka ya Kanisa, kupitia hasa maaskofu wake, katika kufundisha imani na maadili ili kudumisha, kustawisha na kueneza karne hadi karne hazina ya imani iliyofunuliwa na Mungu hasa katika Yesu Kristo na kukabidhiwa kwa Mitume wake.