Urani (uranium) | |
---|---|
Mtapo wa urani
| |
Jina la Elementi | Urani (uranium) |
Alama | U |
Namba atomia | 92 |
Mfululizo safu | Metali |
Uzani atomia | 238.0289 |
Valensi | 2, 8, 18, 32, 21, 9, 2 |
Densiti | 19.1 g·cm³ |
Ugumu (Mohs) | {{{ugumu}}} |
Kiwango cha kuyeyuka | 1405.3 K (1132.2 °C) |
Kiwango cha kuchemka | 4404 K (4131 °C) |
Asilimia za ganda la dunia | 3 · 10-4 % |
Hali maada | mango |
Urani (kwa Kiingereza uranium) ni elementi katika mfumo radidia yenye alama U. Namba atomia ni 92 na uzani atomia ni 238. Atomi yake ina protoni 92 na elektroni 92.
Jina limechaguliwa kutokana na sayari iliyoitwa Uranus kwa kumbukumbu ya mungu mmojawapo wa Dola la Roma.
Urani ni metali nururishi. Isotopi za kawaida katika urani ni urani-238 na urani-235.
Urani ina uzani atomia wa juu kati ya elementi zote zinazotokea kiasili maana yake masi ya atomu yake ni kubwa zaidi. Hata hivyo densiti yake si juu zaidi hivyo mchemraba wa cm³ 1 wa urani ni mwepesi kuliko mchemraba wa cm³ 1 wa dhahabu.
Urani ni metali nyeupe nururishi katika mfululizo wa aktinidi. Isotopi yake 235U ni dutu asilia pekee inayoweza kuwa na mmenyuko mfululizo wa kinyuklia.
Kwa sababu hiyo hutumiwa katika tanuri nyuklia na katika silaha za nyuklia kwa ajili ya vita. Bomu la nyuklia la kwanza lililorushwa juu ya Hiroshima lilitengenezwa kwa urani.