Wilaya ya Muheza

Muheza.

Wilaya ya Muheza ni kati ya wilaya 11 za Mkoa wa Tanga katika Tanzania yenye Postikodi namba 21400.

Makao makuu yapo mjini Muheza.

Mwaka 2012 ilikuwa na wakazi 204,461 walioishi katika kata 33 za wilaya hiyo. Katika sensa ya mwaka 2022 walihesabiwa 238,260 [1].

Wilaya ya Muheza ina ukubwa wa eneo linalokadiriwa kufikia zaidi kilomita za mraba 1470.

Ukiwa katika wilaya hiyo unapata kufika kwenye mitaa na maeneo kama Magila (zamani iliitwa Mbwego), Kisiwani, Majengo Ndani, Majengo Nje, Michungwani, Mdote, Genge, Masimbani, Mbaramo, Masugulu, Shimoni na maeneo ya vijiji kadhaa kama Mkuzi, Mng'aza, Gobo, Bwembwera (Mambo leo, Kilulu, Tongwe, Misozwe, Manyoni, Kicheba, Ubembe, Magoroto (kwenye hifadhi za misitu asilia ya kupendeza), Amani (kwenye hifadhi za misitu asilia ya kupendeza), Moa, Mtimbwane, Mtindiro Mwakijembe, Ngomeni, Nkumba, Pande, Potwe, Songa, Tingeni, Zirai, Mkumbi, enzi, nk

  1. https://www.nbs.go.tz

Wilaya ya Muheza

Dodaje.pl - Ogłoszenia lokalne