Wilaya ya Ukerewe ni wilaya mojawapo kati ya 8 za Mkoa wa Mwanza.
Eneo la wilaya hiyo liko kwenye visiwa vya ziwa Viktoria Nyanza, hasa visiwa viwili vikubwa vya Ukerewe na Ukara pamoja na visiwa vidogo kama vile Kweru, Goziba, Sizu, Irugwa, Kerebe na vingine vingi.