Yako

Mskiti wa Yako

Yako ni mji wa Burkina Faso ya kaskazini na makao makuu ya wilaya ya Passore, katika mkoa wa Nord. Pamoja na vijiji katika eneo lake kuna takriban wakazi 77,000[1].

Iko kilomita 100 kaskazini-magharibi kwa Ouagadougou.

Kihistoria ilijulikana kama mji mkuu wa dola dogo na msikiti mkubwa.

Yako ni mahali ambako rais wa tano wa Burkina Faso Thomas Sankara alizaliwa na kuzikwa.

  1. https://www.citypopulation.de/en/burkinafaso/cities/

Yako

Dodaje.pl - Ogłoszenia lokalne