.
Mlima Elgon ni volkano iliyolala mpakani mwa nchi za Uganda na Kenya [1] kwa upande wa Kenya upo sehemu ya kaskazini mwa Kisumu na magharibi mwa Kitale. Kasoko yake ina kipenyo cha kilomita nane.
Elgon ni mlima wa pili kwa urefu nchini Kenya baada ya Mlima Kenya. Kwa upande wa Uganda ni mlima mrefu mashariki mwa nchi lakini safu milima ya Ruwenzori ni mirefu kuliko mlima Elgon.